Slider


Sports

Life & style

Comments

Fashion

Technology

Blogroll

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Vivamus leo ante, consectetur sit amet vulputate vel, dapibus sit amet lectus. Etiam varius dui eget lorem elementum eget mattis sapien interdum. In hac habitasse platea dictumst.

    

UKUAJI WA MTOTO AKIWA TUMBONI
Hatua ya kwanza ya ukuaji wa Mimba au mtoto akiwa tumboni huanza tangu yai la mama linapokutana na virutubisho toka kwa baba ambapo hutengenezwa kijusi (zygote).

Kuvunjwa vunjwa kwa seli hadi kukamilisha hatua ya kwanza, huchukua kipindi cha wiki kama mbili ndipo kijusi  (zygote) hujikita vizuri  katika mji wa mimba.

Kipindi hiki mwanamke anayetarajia mtoto akipima atagundulika kuwa ni mjamzito na hata yeye mwenyewe huweza kuhisi dalili za mabadiliko.  

Kiini cha Mimba (embryo).
Tangu wiki ya nane  (8) baada ya mimba kutungwa, kipindi hiki kiwango katika kugawanyika kwa seli kunaongezeka.
  Ni kipindi ambacho viungo vya mwili vya kijusi kina anza kutengenezwa
Wakati kijusi kikijishikishiza vizuri katika ukuta wa mji wa mimba, seli zake hutengeneza tabaka mbili. Kwa wakati huu kijusi hubadilika na kuwa kiini cha mimba (embryo).

Tabaka la ndani la kiini hiki  hutengenezwa kuwa mfumo wa kumeng’enya chakula  na mfumo wa hewa.

Tabaka la nje linatengenezwa kuwa mfumo wa fahamu, viungo vya hisia mbalimbali vya mwili huanza kuundwa.

Viungo vya hisia (mfumo wa fahamu) kama masikio, pua, macho na ngozi; nywele na kucha. Sehemu ya katikati hutengenezwa kuwa mifupa, misuli na mfumo wa uzazi. Kimsingi sehemu hii ya kiini cha mimba hutengezwa viungo vya ndani ya mwili.
      

Yanayojiri katika Mji wa Mimba
Baada ya kutengenezwa kwa sehemu kuu tatu za kiini cha mimba, mfumo wa kusaidia ukuaji wa mtoto hutengenezwa sasa.

Mfumo huu ni pamoja na kondo la nyuma, kamba ya kitovu, ambayo huwa na mishipa miwili ya ateri na veini moja ambayo humuunganisha mtoto na kondo la nyuma na fuko la mimba ambalo ndilo hubeba yale maji ambayo ni maalumu kwa kumtunza mtoto hadi atakapozaliwa.

Kimsingi kabla hata mama mtarajiwa hajajua kama ni mjamzito, yote haya yanakuwa yemekuwa yamekwishafanyika katika tumbo lake. Katika wiki ya tatu uti wa mgongo wa mtoto  huanza kutengenezwa.

Katika kipindi cha siku 21, macho huanza kutokeza na siku 24, seli za moyo huanza kujigawanya.

Katika wiki ya nne via vya uzazi huanza kujulikana kama ni kiume au ni kike na vifuko kwa ajili ya mikono na miguu kujitokeza.

Vyumba vinne vya moyo huanza kujitengeza na mishipa ya damu huanza kujitokeza.
       


Tangu wiki ya tano hadi ya nane mikono na miguu huanza kutofautiana na wakati huu pia uso unaaza kutokeza ingawa si rahisi kujulikana.
Katika wiki ya 9 mtoto anakuwa amekua na kufikia urefu wa kama inchi moja hivi. Anakuwa ameshazidi ukubwa wa haragwe ambao alikuwa nao wiki iliyopita. Wakati huu anakuwa ameshaanza kuonyesha viungo.
Pia nikipindi ambacho mtoto anakuwa   kwa haraka sana hadi kufikia  kipindi cha wiki kumi na mbili ambayo ni Sawa na miezi 12.
Ambapo takribani viungo vyote vya mwili vinakuwa  vimesha tengenezwa au kuubwa.
Itaendelea…………

   Je katika kipindi hiki kuna shida gani mama na mtoto anaweza kupata?
   Je nini cha kufanya katika kipindi hiki?
   Je kuna hatari gani iliyopo katika kipindi hiki?
   Je nini hutakiwi kufanya katika kipindi hiki ?
         

    Usisite kuwasiliana nasi
Usisahau kutoa maoni  yako kwa ushauri na maswali kuhusu ujauzito
 Usisite kuwasiliana nasi kwa njia ya WhatsApp namba
  ( 0684127127 - 0762 986 021)

Post a Comment

Translate