Slider


Sports

Life & style

Comments

Fashion

Technology

Blogroll

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Vivamus leo ante, consectetur sit amet vulputate vel, dapibus sit amet lectus. Etiam varius dui eget lorem elementum eget mattis sapien interdum. In hac habitasse platea dictumst.

Aina ya virutubisho vya vyakula kwa mjamzito

Moja kati ya changamoto kubwa ambayo huwakumbuwa wajawazito wengi hata kupelekea watu hao kuweza kujifungua kwa operation ni pamoja na kutokuzingatia lishe ya mama mjamzito, hata hivyo kutokana na changamoto hiyo wengi wa wajawazito wamekuwa wakichagua vyakula vya kula huku wakisahau vile vyakula  walivyoviacha ndivyo vinavyosababisha kukosa lishe kamili ifaayo kwa mama mjamzito.

Zifuatavyo na aina ya vyakula na virutubisho vifaavyo kwa mama mjamzito;

Protini
Protini katika chakula cha mama mjamzito inasaidia ukuaji wa tishu za mtoto, hiyo ni pamoja na ubongo pia hata ogani nyingine za mwili. Pia inasaidia matiti na tishu za tumbo la uzazi kukua wakati wa mimba, na pia inachangia usambazaji mzuri wa damu.

Mama anahitajika kula milo 2 hadi 3 kwa siku yenye vyakula vya protini kama vifuatavyo:-

    Nyama ya ng’ombe ya steki.
    Samaki wa maji baridi au maji chumvi.
    Maini.
    Nyama ya kondoo
    Karanga
    Jamii ya mikunde kama maharage.

Kalshamu (Calcium)
Mama mjamzito anahitaji madini ya kalshamu kama miligramu 1000 kwa siku. Madini ya kalshamu yanasaidia kurekebisha viwango vya majimaji mwilini, kujenga mifupa na meno ya mtoto aliye tumboni.

Vyakula vyenye madini haya ni kama:-
    Mayai.
    Maziwa
    Jibini
    Maharage meupe
    Maharage ya soya
    Samaki
    Kabichi

Madini ya chuma
Madini ya chuma husaidia kuongeza kiwango cha damu mwilini na kukukinga na upungufu wa damu mwilini (Anemia).

Vyakula vyenye madini ya chuma ni kama vifuatavyo:-

    Spinachi
    Mchicha
    Kabichi
    Nyama
    Maini
    Nafaka zisizokobolewa
    Samaki
    Mayai

Folic acid
Folic acid acid hupatikana katika vyakula tunavyokula, hii husaidia kujengeka vizuri kwa ogani za mtoto na kumuepusha na ulemavu pamoja na tatizo linalojulikana kitaalam kama mgongo wazi au neural tube defect (NTD). Katika nchi zinazoendelea mara nyingi wajawazito huwa hawapati virutubisho hivi kwa kiasi cha kutosha katika vyakula, kwa hiyo kinamama wajawazito huongezewa virutubisho hivi kama vidonge vya folic acid wanapohudhuria kliniki.

Folic acid hupatikana katika vyakula kama:-

    Kabichi
    Spinachi
    Machungwa
    Papai
    Limao
    Embe
    Nyanya
    Zabibu
    Tikiti
    Nafaka
    Mkate
    Jamii za mikunde kama maharage

Vitamini C
Matunda na mbogamboga huwa na vitamini C kwa wingi. Vitamini C husaidia uponaji wa majeraha kwa haraka, husaidia meno na fizi na kujengeka kwa mifupa, pia husaidia mmeng’enyo.

Vyakula vyenye vitamini C ni kama:-

    Machungwa
    Limao
    Nyanya
    Zabibu
    Pilipili
    Embe
    Mboga za majani

Tahadhari
Mama mjamzito anatakiwa kuhakikisha kuwa vyakula vyote hivi, lazima viandaliwe katika mazingira safi kuepuka athari kwa mama na mtoto. Vyakula vingine visipopikwa vizuri vyaweza kuwa na vimelea hatari vya magonjwa kama Salmonella na E coli pia aina nyinginezo za vimelea ambavyo vyaweza kuwa hatari kwa afya.

Mpango wa mazoezi
Mpango wa mazoezi ni muhimu kwa mama mjamzito kwa kuwa mazoezi husaidia maendeleo ya kiafya ya mama na mtoto aliye tumboni.Pia mazoezi humsaidia mama kuwa mwenye nguvu wakati wa kujifungua. Mazoezi ya kutembea huwafaa sana kina mama walio wajawazito. Lakini ni vyema kushauriana na daktari wako kabla ya kujihusisha na aina yeyote ya mazoezi.

Post a Comment

Translate